Alhamisi, 16 Oktoba 2014

KATLESI ZA NYAMA YA KUSAGA

Vinavyohitajika

Nyama  ya  kusaga robo kilo

Chumvi

Mbataa   8 za kiasi

Thomu na tangawizi  iliyosagwa

Pili pili  manga  kijiko  cha  chai

Bizari nzima iliyosagwa  nusu kijiko  cha  chai

Mayai  ya  kuchomea

Mafuta  ya  kupikia

Matayarisho

·         kausha  nyama  yako  na  viungo  vyote.
·         iwache  ipoe.
·         menya  mbatata  zako  uzichemshe   na  uziponde  zikisha  wiva(usisahau kutia chumvi unapozichemsha mbatata)
·         zisubiri   zipoe .
·         tengeneza  mviringo  wa  mbatata  ulizoziponda  na  uweke  nyama  yako  kati. 
·         izibe  nyama  yako kwa mchanganyo  wa  mviringo  wako  wa  mbatata  ulizoziponda.
·         teleka  chuma  chako  cha  mafuta  yawache  yapate  moto.
·         lipige  yai  lako  kwenye  kibakuli tia  chumvi  kidogo.
·         chovya  mviringo  wa  katlesi  yako  kwenye  yai  na  uanze  kuchuma.
·         yai  likiwiva  zitoe   na  uweke  kwenye  chujio  zijichuje   mafuta.
·         ukisha  maliza  weka  kwenye  sahani  tayari  kwa  kuliwa.

Kidokezo

 

Unaweza  kutia  kitunguu maji vidogo vidogo  kwenye   nyama  yako  pia  zina kuwa  nzuri.

Pia kotmiri  kwa  wanaopenda  na  hata  pilipili  pia.

Zikiwa  zinapasuka  unapozichoma  usisahau uzigaragaza  kwenye  unga  wa ngano kidogo  ukisha  ndio  uzichove  yai  na  tayari  kwa  kuchomwa

SHARUBATI YA EMBE

Vinavyohitajika

·         Maziwa  lita 2
·         Kibati  cha mango pulp kimoja au embe fresh iliyomenywa unayoweza kupata pulp.
·         Sukari  kiasi

Namna ya kutayarisha na kutengeneza

·         Mimina maziwa kwenye blender.
·         Pamoja na sukari na mango pulp.
·         Isage kwa pamoja  ichanganyike.
·         Imimine kwenye jagi na uweke barafu ya kutosha.
·         Tayari kwa kunywewa.

Kidokezo

Sharbati hii ni nzuri kwa afya na pia unaweza kuifanya kwa matunda tafauti uyapendayo lakini yasiwe ya ukali tu kwani maziwa yatakatika

BANZI ZA MAZIWA

Vinavyohitajika

Unga  wa  ngano  magi 3

Maziwa  ya   maji  magi  1

Hamira  vijiko  2 vya  kulia

Maji  kiasi

Chumvi kijiko 1  cha  kulia

Mafuta  ya  kupikia  au  siagi  vijiko  2 vya  kulia

Namna  ya  kutayarisha

Changanya  unga, hamira, chumvi pamoja  na  maziwa  vichanganye  pamoja.

Ongezea  maji  kidogo  kidogo  mpaka  uchanganyike  na  uuanze  kuukanda.

Ukande   vizuri  mpaka    ukandike   ulainike.

Chukua   tray  zako  upake  mafuta  na   ukate  madonge  ya  unga  upange  kwenye  tray  uwache  uumke   na  uchome  kwenye  oven  gas  mar  7  au  Jiko    la  umeme  200.

Kidokezo

Hakikisha  madonge   ya  unga yasiwe  makubwa  kama  ya   mikate   ya   kusukuma.

MIKATE YA UFUTA YA KIASILI


Vinavyohitajika

Nazi  kipande  1

Nnga  magi  4

Chumvi

Sukari  kijiko  1  ½  cha  chakula

Ute  wa  yai  1

Hamira  vijiko 3  vya  chakula

Ufuta  wa kutosha

Namna  ya  kutayarisha  na  kupika

·         iroweke  nazi  yako  kwenye  blender  kwa  maji  ya  vuguvugu  na  uisage  vizuri
·         weka  unga  wako   ndani  ya  bakuli  na  utie  hamira, chumvi ,sukari  na  ute  wa  yai
·         changanya  unga  wako  kwa  nazi  uliyokwisha  isaga  (tui)
·         upige  unga  wako   (tofauti  na  kuukanda) namaanisha  unga  huu unazidi  maji
·         ukisha  changanyika  vizuri   unga  wako  ufunike  na  usubiri  uumke
·         ukisha  umka
·         weka  bakuli  la  maji  na utie  chumvi  kiasi(lakini  ukiyaonja  chumvi ijitokeze)
·         weka  chuma  chako  kwenye  jiko  kipate  moto  rushia  maji  yenye  chumvi  kwenye chuma  cha  moto
·         teka  unga  wako  kwa kiganja  cha  mkono  una uutandaze  kwenye  chuma 
·         nyunyiza  ufuta  juu ya  mkate  wako  kabla  haujakauka
·         utie kwenye   grill  hapo  utaumuka  na  kuwiva  kuwa  rangi  nzuri  ya  kuvutia
·         rejesha  tena  juu  ya  jiko  kwa moto  wa kiasi  na  uupake  mafuta  kwa  brash 
·         utoe  na  uuweke  sahanini  tayari  kwa  kuliwa.

Kidokezo

Ukitia  yai  na kiini  chake  cha  manjano  utachelewa  kuumka  na  hautakuwa  na  rangi nzuri  ya   kuvutia

MSETO

Vinavyohitajika

·         Choroko zilizopaazwa magi 1
·         Nazi ya kipande ½ (cream coconut)
·         Mchele magi 1
·         Chumvi

Namna ya kutayarisha na kupika

·         Roweka choroko kwa muda wa masaa 2 kwenye maji ya vuguvugu.
·         Injika sufuria ya maji kwenye jiko na usubiri yachemke sawa sawa na uzigide maji choroko zako na uzitie kwenye maji hayo yanayochemka.
·         Pia roweka mchele  kwenye maji ya kawaida.
·         Choroko zikishawiva utaziona zimeachana kiasi cha kwamba ukizishika kwa vidole zinavurugika bila ya kutumia nguvu .
·         Gida maji mchele na umimine kwenye mchemko wa choroko.
·         Weka chumvi kiasi.
·         Isage nazi kwa kutumia maji ya vuguvugu na uhakikishe imesagika na kutoa tui lililokuwa zito kiasi cha 1/2 ya magi yako.
·         Irudie kuisaga tena nazi  kwa kipimo cha maji magi 1
·         Mchanganyiko wa mchele ukishawiva vizuri, weka tui la nazi  ya kipimo cha magi1.
·         Kifunike chakula mpaka maji yawe yamekauka na uanze kuusonga mseto ili upate kuchanganyika vizuri na uweke lile tui lako zito la mwanzo ambalo ni ½ magi. Usonge vizuri na upambie kwa muda wa dakika 10 na uupakue kwenye sahani na tayari kwa kuliwa.

Kidokezo

Mseto usiuwache ukauke sana kwa sababu kila ukikaa unazidi kujishika na kuwa mgumu kwani unapendeza kuliwa ukiwa mlaini kidog

Egg roll

Vinavyohitajika

1.   Nyama  ya  kusaga  ¼  kilo
2.   Mayai  4  makubwa
3.   Papi  za  sambusa  3
4.   Chumvi
5.   Pilipili  mtama (manga) ½  kijiko  cha  kula
6.   Pilipili  boga  ¼ 
7.   Kotmiri  ½  ya  kisahani  cha  chai
8.   Thomu  na   tangawizi  kijiko  1  cha  chai
9.   Ndimu  kijiko  1  cha  chai
10.                Unga  wa  toast (bread  crumble)
11.                Mafuta  ya  kupikia

Namna  ya  kutayarisha 

·         Katakata  pilipili boga  vipande  vidogo vidogo. 
·         Chambua  majani  ya  kotmiri .
·         Kausha  nyama  yako  kwa  kutia thomu na  tangawizi, pilipili manga,chumvi  pamoja na  ndimu.
·         Iwache  ipoe.
·         Piga  mayai  yako 3  kama  kiwanda  uyamimine  kwenye  chuma  cha  mafuta  ya moto (weka  kijiko  kimoja  na  nusu  cha  chakulia).
·         Tandaza  nyama  yako  ndani  kiwanda  na  utie   pilipili  boga  juu  yake  na ikifuatiwa  na  kotmiri.
·         Kigeuze  kiwanda  chako  upande  wa  pili  na   uhakikishe  kimewiva  vizuri.
·         Ukisha  maliza  kupika  kiwanda. 
·         Weka  kaki zako  kwa  mpangilio   ufuatao:-
1.   Weka  papi  yako  ya  kwanza  na  uipake  ute  wa yai  pembezoni.
2.   Na   weka  papi yako  ya  pili  juu   yake  zishikane.
3.   Paka  tena  ute  wa  yai  mwisho  wa  papi  zako  mbili
4.   Weka  kaki  yako  ya  tatu  mwisho  wa  kaki  yako  ya   pili  ili  zishikane  upate urefu  unaohitajika
·         Kiweke  kiwanda  chako  juu ya  kaki  zako  mbili  ulizounganisha  mwanzo.
·         Anza  kuroll  mpaka  mwisho  na  hakikisha  unapata  mviringo  uliokaa  sawa.
·         Tayari  kwa  kukata  slice  za  mviringo  huo.
·         Paka  mviringo  wako yai  pembeni.
·         Ugaragize  kwenye  unga  wa  toast.
·         Anza  kuzichoma  egg rolls  zako  kwa  moto mdogo mdogo   kwenye  chuma cha   kuchomea  lakini  usiweke  mafuta  mengi  ( weka  vijiko  vya  chakula  4 vya  mafuta  kwa  kila  egg roll  8).

·         Vitowe  na  tayari  kwa  kuliwa

Kidokezo

Ni vizuri  kuhimiza  kuvikata wakati  yai  likiwa  limoto  na  kaki  kabla  ya  kukauka  kwani ukichelewa  utapata  tab

Keki ya kawaida

Keki ya Kawaida
 
Vinavyohitajika

·         Siagi ya baking 500g – nusu kilo.
·         Sukari 500g – nusu kilo.
·         Unga  wa ngano 1000g – kilo moja.
·         Arki rose kijiko 1 cha kulia chakula.
·         Arki vanilla kijiko 1 cha kulia chakula.
·         Baking powder vijiko 2 vya kulia chakula.
·         Cocoa au unga wa kahawa vijiko 3 vya kulia chakula.
·         Unga wa mdalasini kijiko 1 cha chai.
·         Mayai yakiwa makubwa 10 na yakiwa madogo 12.
·          Baking tray - Tray ya Kuokea.

namna  ya kutayarisha

·         Weka siagi ndani ya bakuli la kuchanganyia  pamoja na sugari  uichanganye  pamoja mpaka vichanganyike  vizuri (unaweza kuisaga  sukari yako ukitaka lakini si lazima).
·         Ikichanganyika vizuri weka mayai uchanganye pamoja pia  ichanganyike  vizuri.
·         Weka arki zote mbili kwa pamoja huku  ukizichanganya
·         Uchanganye unga na baking powder na uanze kuweka kwenye mchanganyiko wa siagi, mayai  na sukari.
·         Hakikisha unaweka unga wako kidogo kidogo na sio wote kwa wakati mmoja.
·         Ukisha changanyika punguza  mchanganyiko huo robo yake kwenye bakuli jengine na utie unga wa Cocoa au kahawa pamoja na mdalasini na uchanganye  vizuri mpaka ubadilike uwe rangi moja.
·         Ipake  siagi  kwenye baking tray na umimine mchanganyiko wa keki  ambayo haina cocoa robo ya unga na utandaze vizuri.
·         Weka mchanganyiko wako wenye cocoa juu yake pia utandaze vizuri.
·         Malizia kwa kuweka mchanganyiko wa keki iliyokuwa haina cocoa kwa juu tandaza vizuri na tayari kwa kuichoma.
·         Kwa wanaotumia jiko la Gesi ni kipimo cha mark 5 na kwa wale wanotumia jiko la umeme ni mark 250 ya spidi ya jiko.
·         Ili iwive vizuri na kuwa na rangi ya kupendeza inachukua muda wa saa 1  kuokwa na tayari kwa kuliwa.

Kidokezo

Unaweza kutumia mashine ya kusagia keki na kama huna  tumia mwiko tu kwa kuchanganyia na itakuwa nzuri tu usikhofu. Pia isubiri keki  ipoe ndio uitowe kwa kuhofia isije ikakatika wakati wa kuitoa kwenye  tray ya kuokea - baking tray.

UROJO

Mbatata za Urojo

 
 
Vinavyohitajika

Mbatata  ¼ kilo

Bizari ya manjano ¼ kijiko cha chakula

Ndimu 1 kubwa

Embe mbichi moja

Chumvi

Unga wa ngano vijiko vya chakula 4

Namna ya kutayarisha na kupika

Chemsha mbatata na maganda yake

Zikishawiva, ziepue na uziwache zipoe

Teleka sufuria ya maji kwenye jiko lenye moto pamoja na embe mbichi

Koroga unga kwa maji na bizari uwe kama wa kupikia uji

Maji yakianza kupata moto weka unga na upike kama uji

Uwache uchemke na huku ukiukoroga

Kamua ndimu uweke kwenye urojo pamoja na chumvi

Zimenye mbatata na uzikate vipande vidogo vidogo uweke kwenye bakuli na umimine urojo tayari kwa kuliwa.

Kidokezo

Zinapendeza kuliwa kwa mishikaki ya kuku au nyama. Pia bajia ndio mwenziwe pia usikose chips za muhogo na kachori.