Alhamisi, 16 Oktoba 2014

MSETO

Vinavyohitajika

·         Choroko zilizopaazwa magi 1
·         Nazi ya kipande ½ (cream coconut)
·         Mchele magi 1
·         Chumvi

Namna ya kutayarisha na kupika

·         Roweka choroko kwa muda wa masaa 2 kwenye maji ya vuguvugu.
·         Injika sufuria ya maji kwenye jiko na usubiri yachemke sawa sawa na uzigide maji choroko zako na uzitie kwenye maji hayo yanayochemka.
·         Pia roweka mchele  kwenye maji ya kawaida.
·         Choroko zikishawiva utaziona zimeachana kiasi cha kwamba ukizishika kwa vidole zinavurugika bila ya kutumia nguvu .
·         Gida maji mchele na umimine kwenye mchemko wa choroko.
·         Weka chumvi kiasi.
·         Isage nazi kwa kutumia maji ya vuguvugu na uhakikishe imesagika na kutoa tui lililokuwa zito kiasi cha 1/2 ya magi yako.
·         Irudie kuisaga tena nazi  kwa kipimo cha maji magi 1
·         Mchanganyiko wa mchele ukishawiva vizuri, weka tui la nazi  ya kipimo cha magi1.
·         Kifunike chakula mpaka maji yawe yamekauka na uanze kuusonga mseto ili upate kuchanganyika vizuri na uweke lile tui lako zito la mwanzo ambalo ni ½ magi. Usonge vizuri na upambie kwa muda wa dakika 10 na uupakue kwenye sahani na tayari kwa kuliwa.

Kidokezo

Mseto usiuwache ukauke sana kwa sababu kila ukikaa unazidi kujishika na kuwa mgumu kwani unapendeza kuliwa ukiwa mlaini kidog

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni