Alhamisi, 16 Oktoba 2014

KATLESI ZA NYAMA YA KUSAGA

Vinavyohitajika

Nyama  ya  kusaga robo kilo

Chumvi

Mbataa   8 za kiasi

Thomu na tangawizi  iliyosagwa

Pili pili  manga  kijiko  cha  chai

Bizari nzima iliyosagwa  nusu kijiko  cha  chai

Mayai  ya  kuchomea

Mafuta  ya  kupikia

Matayarisho

·         kausha  nyama  yako  na  viungo  vyote.
·         iwache  ipoe.
·         menya  mbatata  zako  uzichemshe   na  uziponde  zikisha  wiva(usisahau kutia chumvi unapozichemsha mbatata)
·         zisubiri   zipoe .
·         tengeneza  mviringo  wa  mbatata  ulizoziponda  na  uweke  nyama  yako  kati. 
·         izibe  nyama  yako kwa mchanganyo  wa  mviringo  wako  wa  mbatata  ulizoziponda.
·         teleka  chuma  chako  cha  mafuta  yawache  yapate  moto.
·         lipige  yai  lako  kwenye  kibakuli tia  chumvi  kidogo.
·         chovya  mviringo  wa  katlesi  yako  kwenye  yai  na  uanze  kuchuma.
·         yai  likiwiva  zitoe   na  uweke  kwenye  chujio  zijichuje   mafuta.
·         ukisha  maliza  weka  kwenye  sahani  tayari  kwa  kuliwa.

Kidokezo

 

Unaweza  kutia  kitunguu maji vidogo vidogo  kwenye   nyama  yako  pia  zina kuwa  nzuri.

Pia kotmiri  kwa  wanaopenda  na  hata  pilipili  pia.

Zikiwa  zinapasuka  unapozichoma  usisahau uzigaragaza  kwenye  unga  wa ngano kidogo  ukisha  ndio  uzichove  yai  na  tayari  kwa  kuchomwa

Maoni 4 :