Jumatatu, 29 Septemba 2014

BIRIANI YA SAMAKI

MAHITAJI:

Mchele 1kg

Samaki 1kg

Vitunguu maji 1kg

Samli kiasi

Thomu

Mmdalasini

Hiliki

Ndimu

Nyanya

Chumvi kiasi

Njia:

1. Mkatekate samaki umtie chumvi ndimu umkaange. Menya vitunguu
uvikate. Saga nyanya. Thomu na viungo vyote vilivyosalia. (bakisha
mdalasini nzima kidogo)

2. Teleka sufuria utie samli, ikichemka tia vitunguu uvikaange,
vikianza wekundu tia nyanya na viungo kidogo. Acha vikaange kwa
muda mdogo halafu tia vipande vyote vya samaki, chumvi na ndimu,
pamoja na maji kidogo. Acha ichemke kwa muda mdogo ibaki na rojo
rojo epua.

3. Chukuwa sufuria nyengine uitie maji na chumvi. Yakichemka osha mchele
utie. Acha utokote. Angali kiini wali. Ukiona umewiva umimine uyachuje
maji yote. Teleka tena sufuria pamoja na vile viungo ulivyovisaga. Vyote
vikaange kidogo halafu umimine wali wote ukorogekoroge ili upate
kuchanganyika na viungo. Halafu uweke vizuri upalie moto. Ukishakauka
utaupakuwa. Kuupakuwa kwake utatia wali sahani, baadae ndio utatia
samaki pamoja na rojo rojo zake kwa juu.

VILEJA VYA CHUMVI

MAHITAJI:

Siagi *

Unga wa ngano 1kg

Mayai 2

Jam

Njia:

Changanya unga na siagi mpaka uchanganyike sawa sawa, kama mgumu tia
maji baridi kidogo. Kata nakshi uipendayo huku ukipaka yai na jam juu yake.
Choma na wacha vipoe.

TOFI

MAHITAJI:

Maziwa ya kibati

Maji * kikombe

Hiliki

Sukari na arki kiasi

Njia:

Teleka maziwa changanya maji, sukari arki na iliki koroga usiwache mkono
mpaka iwe nzito. Tia samli kidogo na epua. Tandaza kwenye sinia
iliyopakwa samli na kata.

FARNE


MAHITAJI:

Unga wa mchele

Maziwa yaliyochemshwa

Iliki na sukari

Njia:

Teleka maziwa na yakichemka tia sukari na iliki wacha yachemke tena
kidogo. Tia unga uliovurugwa kwa maji na wacha uchemke kidogo. Ukiwiva
epua na mimina ndani ya bakuli. Wacha ipoe na kata vipande. Tayari kwa
kula.

VIKONI

MAHITAJI:

Unga wa ngano

Pilipili manga

Chumvi

Siagi

Nyama ya kusaga iliyochemshwa na kutiwa viungo.

NJIA :

Changanya unga na samli, chumvi na pilpili manga mpaka vichanganyika na
kua kitu kimoja kata madonge na sukuma kwenye kibao.Kata kwa umbo la
duara na weka nyama yako katikaati. Pasua kidogo kwa kisu pinda duara na
ikae kama koni na nyama itokeze juu. Choma kwa oven au kwa makaa na
vikikaribia wekundu epua.

KITAWA


MAHITAJI:
Ndizi mbichi 6

Chumvi

Maziwa ya mgando

Njia:

Menya ndizi na kata vipande vifupi. Safisha ndizi vizuri hadi utomvu utoke,
kisha zichemshe hadi zilainike vizuri, ziponde kisha zichanganye na maziwa
ya mgando hadi kuwa kama uji mzito. Pakua na andaa.

KARI YA SAMAKI

MAHITAJI:

Mnofu wa samaki4oz

Nyanya 1

Kitunguu maji

Thomu

Bizari

Limau

Maziwa fresh

Mafuta ya maji.

NJIA

Safisha samaki na kata vipande.Menya na katakata vitunguu,na ponda
vutunguu thomu.Osha na menya nyanya ikate vipande vidogovidogo. Pasha
moto mafuta na kaanga vitunguu. Ongeza viungo vyengine na endelea
kukaanga. Ongeza nyanya na endelea kukaanga, zikilainika ongeza samaki
na maziwa na endelea kupika taratibu kwa muda wa dakika 10-15. Ongeza
maji ya limau na endelea kutokosa kwa dakika 3 zaidi. Epua na andaa.

VICTORIA SANDWICH

MAHITAJI:

Unga wa ngano 6oz

Mayai 4

Jam vijiko vya mezani 2

Siagi 4oz

Chumvi mziwa kidogo.

Njia:

Saga mchanganyiko wa sukari na siagi hadi uwe laini na mwepesi kidogo,
pasua mayai na pigapiga na ongeza kwenye mchangayiko kidogo kidogo.
Chekecha unga, chumvi na changanya kwenye mchangayiko kidogo kidogo.
Ongeza maziwa hadi mchangayiko uwe mweupe kidogo (unaomiminika) Paka
mafuta legeni 2 na weka mchanganyiko wa keki kwenye legeni zote. Oka
kwa dakika 20 kwenye oven.

Keki ikiiva epua na acha ipoe. Paka jam juu ya keki moja sehemu ya chini na
shikamanisha na keki ya pili. Nyunyiza sukari laini juu au pamba
upendavyo.

LEMON BISCUITS

MAHITAJI:

Unga wa ngano 4oz

Siagi 2oz

Kiini cha yai 1

Sukari 2oz

Ganda la limiau lililokunwa.

Njia:

Paka legeni mafuta, chekecha unga na fikicha siagi hadi mchanganyiko
ufanane na chenga za mkate. Ongeza sukari na ganda la limau. Ongeza kiini
cha yai lililopigwa, ongeza na maji baridi kidogo hadi kiwe laini na kufaa
kusukumwa, sukuma kinyunga hadi kiwe na unene wa 3 kata mviringo ya
biscuits na weka kwenye legeni. Toboa mashimo ya urembo oka biskuti
kwenye oven zikiwiva epua na nyunyiza sukari ukipenda.

PAI YA NYAMA


MAHITAJI:
Nyama ya kusaga oz 6

Karoti 1

Kitunguu 1

Nyanya 1

Giligilani 2tsp

Chumvi 1 tsp

Yai lililopigwa

Maziwa 2oz

Siagi 2tsp

Viazi mviringo vilivyopikwa na kupondwa 6oz.

Njia:

Pika nyama hadi iwive, Menya kitunguu na karoti na kata vipande vidogo
vidogo. Menya nyanya na katakata, pasha mafuta moto na kanga viungo
vyote, ongeza nyama na maji kidogo visiwe vikavu sana, Ponda viazi vingali
moto ongeza siagi, maziwa na chumvi, Paka mafuta chombo cha kuwekea
pai (pai dish) na weka mchanganyiko wa nyama ndani. Tandaza viazi juu ya
nyama. Sawazisha kwa kisu. Tengeneza viumbo lolote juu ili kupamba. Paka
yai juu ya viazi kisha oka kwenye oven yenye joto 160deg C. hadi pai iwe
kahawia. Epua na andaa pamoja na mchuzi rojo. N.B. unaweza kupaka
maziwa juu badala ya yai.

PAI YA SAMAKI

MAHITAJI:

Samaki oz 12 (minofu iliyochemshwa)

Viazi vidogo 3 vilivyochemshwa

Nyanya ndogo 3

Macaroni oz 2, (yaliyochemshwa na kupakwa siagi, chumvi, Jimbini 2 oz

Pilipili ya ungaa * tsp

Siagi oz 1

Mayai 2

Maji yaliyochemshiwa samaki * kikombe

Chenga za mkate oz 1.

Njia:

Paka mafuta kidogo, piga piga mayai ndani ya bakuli na ongeza minofu ya
samaki yalichambuliwa na nusu ya viazi vilivyopondwa, chumvi, pilipili na
macaroni, ongeza mchuzi wa samaki na changanya vizuri. Pakua nusu ya
mchanganyiko ndani ya pie dish. Panga nyanya zilizokatwa slice za * ikisha
ongeza mchanganyiko uliobaki na panga tena nyanya zilizobaki. Funika na
mchanganyiko wa viazi vilivyobaki.

Nyunyiza jibini na chenga za mkate juu ya pie kisha paka (dondosha) siagi
kidogo kidogo juu yake. Oka katika oven yenye joto 125-150 deg.C. mpaka
pie iwive na iwe rangi ya kahawia epua.

FISH ROLL

MAHITAJI:
Samaki 2 wabichi waliochemshwa

Viazi mviringo vilivyochemshwa na kupondwa

Siagi tsp 1

Yai lililopigwa

Chenga za mkate

Maziwa fresha 2tsp

Chumvi 1 tsp

Chumvi 1tsp

Pilipili ya unga

Njia:

Ondoa ngozi na mifupa kwenye samaki na chambua minofu. Ongeza viazi
vilivyopondwa na siagi, ongeza pili pili na chumvi, ongeza nusu ya yai na
changanya vizuri kama mchanganyiko ni mkavu ongeza maziwa, changanya
vyema na tengeneza mviringo mirefu 4, pakaza yai lililobakia na viringisha
samaki (rolls) kwenye chenga za mkate. Paka legeni mafuta na kuoka rolls
kwenye oven na joto 170 – 180 degrees F. kwa muda wa dakika 20 – 25.
andaa pamoja na tomato sauce.

N.B waweza kukaanga rolls kwenye mafuta (kwa kutosa) hadi iwe rangi
kahawia na hudhurungi baada ya kuokwa.

MEAT CURRY

MAHITAJI:

Nyama oz 8

Bizari oz 1

Vitunguu 3 vilivyolengwa

Pilipili 1

Thomu tembe 2

Tangawizi iliyosagwa

Mafuta ya maji oz 2

Nazi1

Limau1/4.

Njia

1. Safisha nyama na kata vipande vidogovidogo.

2. Ongeza kitunguu thomu, thangawizi na bizari kwenye nyama
changanya vizuri iwache kwa muda viungo vikolee.

3. Kamua na chuja tui la nazi mara tatu.

4. Pasha moto mafuta na kaanga vitunguu hadi viwive, Ongeza vitunguu
na nyanya na endelea kukaanga kwa dakika2

5. Ongeza tui la nazi ulilokamua mara ya pili na tatu changanya vizuri
na koroga na acha ichemke.Ongeza tui la kwanza,punguza moto na
kuacha nyama iendelee kutokota.

6. Epua na ongeza kijiko kidogo cha maji ya limau koroga vuzuri na
andaa.

Kari ya nyama yaweza kuandaliwa na wali au mkate.

SAMAKI WA KUKAANGA

MAHITAJI:

Minofu 2 ya samaki mbichi

Yai 1 piga

Chumvi kiasi

Mafuta

Maji tbl sp 2

Chenga za mkate tb. Sp 2

Njia :

1. Osha minofu ya samaki ikaushe maji na ipake chumvi na pilipili.

2. Weka vipande vya samaki kwenye yai na vibinginishe kwenye
chenga za mkate.

3. Kaanga minofu ya samaki hadi iive na ibadilike rangi ya kahawia.epua
andaa

DINNER ROLL

DINNER ROLLS

Unga wa ngano 8oz

Sukari tsp 1

Siagi 1oz

Chumvi tsp1

Hamira tsp 1

Maziwa ya uvugu uvugu kikombe 1

Yai 1

Njia:

Chekecha unga na chumvi kwenye bakuli kubwa

Fikicha siagi na unga

Tengeneza shimo katikati ya unga na tia sukari na hamira. Changanya ili
kufanya uji mwepesi sana. Funika na weka mahali pa uvugu uvugu kwa muda
wa dakika 10-15.

Hamira ikisha umuka changanya unga na maziwa au maji ya uvugu na fanya
kinyunga kanda kiunga vizuri na bila kuongeza unga ikiwezekana.

Acha kinyunga kiumuke mara mbili ya ukubwa wake kisha kanda tena.

Tengeneza maumbo mbali mbali kisha acha ili uumuke tena weka kwenye
legeni.

Piga piga yai kisha paka juu ya rolls oka kwenye oven yenye joto 300F –
350F au 170C – 180C kwa muda wa dakika 15-20 epua.

JAM BUNS

JAM BUNS/ANDAZI LA JAM

Unga wa ngano 8oz

Hamira ya unga vijiko vya chai tsp2

Mayai 2

Jam vijiko vya kulia 2

Siagi vijiko vya kulia 2

Sukari vijiko vya kulia 4

Maziwa * kikombe

Njia:

Chekecha unga na hamira kwenye bakuli kubwa

Fikicha siagi na unga hadi mchanganyiko ufanane na chenga za mkete.

Ongeza sukari na changanya vyema.

Ongeza yai lililopigwa mara 2 na maziwa na changanya vyote vizuri ili kuwe
na donge laini. Washa oven 250F-300F au 140C-150C.

Tengeneza shimo katikati ya kinyunga kwa kidole na weka juu jam kidogo.

Tengeneza vimviringo vidogo vidogo kwa kiganja cha mkono.

Paka mafuta legeni na weka vile vimviringo kwenye legeni.

Oka kwenye Oven kwa muda wa dakika 15 – 20

Epua na tayarisha

MEAT CAKE

MEAT CAKE

Nyama 11/2kg (ya kusaga)

Siagi 1/4kg

Unga1/4kg

Carrot1/4kg

Pilipili mbuzi 1/4kg

Mayai 18

Uzile

Mdalasini

Pili pili manga

B.powder 2tsp

Ndimu 1

Thomu kidogo

Method:

Changanya nyama, thomu, ndimu, pilipili manga, mdalasini na uzile na upike
pamoja iwive kasha saga siagi na mayai 6 hadi iwe cream na nyepesi kama
unavyofanya kwa keki ya sukari kasha changanya pamoja kwa unga na
B.powder changanya kwa mkono mpaka uchanganyike piga mayai mengine 6
na uchanganye na ile nyama kwa kijiko mpaka ichanganyike vizuri. Para
carrot zako kwa kutumia kile kibati cha kuparia chips nazo ziwe kama chips
tena zichemshe kidogo ziwive, kata pilipili boga ziwe slices za duara
nyembamba. Mwisho paka trey yako siagi itandaze ienee yote na mimina ule
mchanganyiko wa cake juu yake halafu tandaza juu yake ule mchanganyiko
wa nyama na mayai, tena vunja mayai 6 yalibakia uyapige vizuri, tandaza
carrots zako juu yake na zile slices za pili pili boga, kasha malizia kwa
kunyunyiza mote yale mayai uliyoyapiga tia ktk oven pre-heated temp. 180C
mpaka ikauke na iwive na ikipoa kata square na uwandae.

Jumapili, 28 Septemba 2014

HALF CAKE

Mapishi ya Half cake (Keki)

Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2
Sukari (sugar) 1/4 kikombe
Barking powder 1/2 kijiko cha chai
Magadi soda (bicarbonate soda) 1 kijiko cha chai
Mafuta 2 vijiko vya chai
Mafuta ya kukaangia
Maji ya uvuguvugu kiasi

Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa

Jumamosi, 27 Septemba 2014

JUICE YA UBUYU

Mahitaji
Ubuyu(wa unga au wa mbegu)
Maji
Sukari
Njia:
1.Chambua ubuyu,ondo uchafu wowote uliopo kwenye ubuyu
2.Katika sufuria,weka ubuyu kisha ongeza maji.Katika kila kipimo cha ubuyu ongeza maji mara tatu yake
Ubuyu wa mbegu vikombe 6  weka maji vikombe 9
Ubuyu wa unga  vikombe 3 weka maji vikombe 12
3.Funika sufuria kisha bandika jikoni,chemsha adi vitokote,vipe  angalau dakika nne za kutokotea.
 
Kumbuka maji unayotumia kuchemsha ubuyu ni maji ya bomba na si salama,hivyo ni muhim kuyapa  muda mzuri wa kuchemka ili juice yako iwe salama.
4.Juisiinapoanza tu kutokota ongeza sukari kwa ladha uipendayo kisha acha zile dakika nne za kutokota ziishe.Zima jiko acha juisi ipoe.
Napenda kuweka sukari ichemkie kwenye juice kwani inafanya juice ishikane na kua nzito.Sukari ikichemshwa inakawaida ya kua nzito.Kumbuka kwamba ubuyu ni mwepesi sana na juice yake kawaida hujitenga inapotulia,ubuyu waenda chini na maji yanabaki juu.Ukichemsha sukari inasaidia kuondoa hali hiyo.
5.Chuja juisi,ongeza maji kama unaona ni nzito sana,na ongeza sukari endapo ile uliyoweka awali haitoshi.Juisi tayari kwa kunywa

Pilau Ya Nyama Ya Ng'ombe Na Nyanya






Vipimo

Mchele (Basmati)                                          3 vikombe

Nyama ya ngo’mbe                                      1 kg

Pilipili boga                                                    1 kubwa

Nyanya                                                        2 kubwa

Vitunguu maji                                               2 vikubwa

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa       1 kijiko cha supu

Tangawizi                                                     1 kijiko cha chai

Ndimu                                                          1

Mafuta ya kupikia                                         ½ kikombe

Mdalasini                                                      ½  kijiko cha chai

Binzari nyembamba                                      1 kijiko cha chai

Pilipili manga                                                  ½ Kijiko cha chai

Hiliki                                                             ½ Kijiko cha chai


Namna ya kutayarisha na Kupika


Roweka mchele wako katika chombo


Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi


Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi


katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni


Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia


Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto


Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya


Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi


Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke


Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza


Funika na punguza moto na uache uive taratibu


Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.

Jumatatu, 22 Septemba 2014

karibuniii

Karibuni katika blog yetu ya mapishi.Hapa mtajifunza mengi yahusuyo mapishi.