Jumatatu, 29 Septemba 2014

PAI YA SAMAKI

MAHITAJI:

Samaki oz 12 (minofu iliyochemshwa)

Viazi vidogo 3 vilivyochemshwa

Nyanya ndogo 3

Macaroni oz 2, (yaliyochemshwa na kupakwa siagi, chumvi, Jimbini 2 oz

Pilipili ya ungaa * tsp

Siagi oz 1

Mayai 2

Maji yaliyochemshiwa samaki * kikombe

Chenga za mkate oz 1.

Njia:

Paka mafuta kidogo, piga piga mayai ndani ya bakuli na ongeza minofu ya
samaki yalichambuliwa na nusu ya viazi vilivyopondwa, chumvi, pilipili na
macaroni, ongeza mchuzi wa samaki na changanya vizuri. Pakua nusu ya
mchanganyiko ndani ya pie dish. Panga nyanya zilizokatwa slice za * ikisha
ongeza mchanganyiko uliobaki na panga tena nyanya zilizobaki. Funika na
mchanganyiko wa viazi vilivyobaki.

Nyunyiza jibini na chenga za mkate juu ya pie kisha paka (dondosha) siagi
kidogo kidogo juu yake. Oka katika oven yenye joto 125-150 deg.C. mpaka
pie iwive na iwe rangi ya kahawia epua.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni