Jumatatu, 29 Septemba 2014

JAM BUNS

JAM BUNS/ANDAZI LA JAM

Unga wa ngano 8oz

Hamira ya unga vijiko vya chai tsp2

Mayai 2

Jam vijiko vya kulia 2

Siagi vijiko vya kulia 2

Sukari vijiko vya kulia 4

Maziwa * kikombe

Njia:

Chekecha unga na hamira kwenye bakuli kubwa

Fikicha siagi na unga hadi mchanganyiko ufanane na chenga za mkete.

Ongeza sukari na changanya vyema.

Ongeza yai lililopigwa mara 2 na maziwa na changanya vyote vizuri ili kuwe
na donge laini. Washa oven 250F-300F au 140C-150C.

Tengeneza shimo katikati ya kinyunga kwa kidole na weka juu jam kidogo.

Tengeneza vimviringo vidogo vidogo kwa kiganja cha mkono.

Paka mafuta legeni na weka vile vimviringo kwenye legeni.

Oka kwenye Oven kwa muda wa dakika 15 – 20

Epua na tayarisha

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni