Jumatatu, 29 Septemba 2014

BIRIANI YA SAMAKI

MAHITAJI:

Mchele 1kg

Samaki 1kg

Vitunguu maji 1kg

Samli kiasi

Thomu

Mmdalasini

Hiliki

Ndimu

Nyanya

Chumvi kiasi

Njia:

1. Mkatekate samaki umtie chumvi ndimu umkaange. Menya vitunguu
uvikate. Saga nyanya. Thomu na viungo vyote vilivyosalia. (bakisha
mdalasini nzima kidogo)

2. Teleka sufuria utie samli, ikichemka tia vitunguu uvikaange,
vikianza wekundu tia nyanya na viungo kidogo. Acha vikaange kwa
muda mdogo halafu tia vipande vyote vya samaki, chumvi na ndimu,
pamoja na maji kidogo. Acha ichemke kwa muda mdogo ibaki na rojo
rojo epua.

3. Chukuwa sufuria nyengine uitie maji na chumvi. Yakichemka osha mchele
utie. Acha utokote. Angali kiini wali. Ukiona umewiva umimine uyachuje
maji yote. Teleka tena sufuria pamoja na vile viungo ulivyovisaga. Vyote
vikaange kidogo halafu umimine wali wote ukorogekoroge ili upate
kuchanganyika na viungo. Halafu uweke vizuri upalie moto. Ukishakauka
utaupakuwa. Kuupakuwa kwake utatia wali sahani, baadae ndio utatia
samaki pamoja na rojo rojo zake kwa juu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni