Jumatatu, 29 Septemba 2014

MEAT CURRY

MAHITAJI:

Nyama oz 8

Bizari oz 1

Vitunguu 3 vilivyolengwa

Pilipili 1

Thomu tembe 2

Tangawizi iliyosagwa

Mafuta ya maji oz 2

Nazi1

Limau1/4.

Njia

1. Safisha nyama na kata vipande vidogovidogo.

2. Ongeza kitunguu thomu, thangawizi na bizari kwenye nyama
changanya vizuri iwache kwa muda viungo vikolee.

3. Kamua na chuja tui la nazi mara tatu.

4. Pasha moto mafuta na kaanga vitunguu hadi viwive, Ongeza vitunguu
na nyanya na endelea kukaanga kwa dakika2

5. Ongeza tui la nazi ulilokamua mara ya pili na tatu changanya vizuri
na koroga na acha ichemke.Ongeza tui la kwanza,punguza moto na
kuacha nyama iendelee kutokota.

6. Epua na ongeza kijiko kidogo cha maji ya limau koroga vuzuri na
andaa.

Kari ya nyama yaweza kuandaliwa na wali au mkate.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni